Powered By Blogger

Saturday, April 16, 2011

MTOTO WA CHINA ATEULIWA KUWA BALOZI WA MAPINDUZI YA KIJANI WA UMOJA WA MATAIFA

Mtoto Li Hongyan akifurahia uteuzi wake kama Balozi mdogo kuliko wote wa Mapinduzi ya Kijani Duniani huko katika Makao Makuu ya UN Habitat, jijini New York, Marekani
  

    Li Hongyan binti kutoka nchini China ameteuliwa kuwa Balozi wa Umoja huo wenye nchi wanachama wengi kuliko yote duniani katika harakati zake za kutunza mazingira ( Green Revolution).
    Li 7, ambaye ndio amewahi kuwa mwakilishi mdogo kuliko wote katika historia ya Umoja huo. Anahamasisha jamii inayomzunguka kwa kuhodhi mapinduzi hayo muhimu kwa mintaarafu ya kuilinda dunia yetu dhidi ya majanga.
    Akiongea baada ya kupokea wadhifa huo wa heshima Li anadai kuwa angependa kuwafundisha wanafunzi wenzie maarifa hayo ili wapita njia wapate kushangaa pindi wapitapo karibu na mazingira hayo.
    Naye Rais wa Uga huo wa sita amesifia sana juhudi za Wachina kuhamasisha watoto wao dhidi ya utunzaji wa mazingira . Anaamini kuwa vitendo vya mtoto kama Li vitahamasisha watoto wengine kupigania mapinduzi hayo,
 
    Je, wako wapi watoto kama akina Li kutoka bara Afrika?

    "Nyota njema huonekana asubuhi"
                                   Msemo wa Kisuaheli

No comments:

Post a Comment