Powered By Blogger

Friday, April 22, 2011

CHANGAMOTO KWA VIONGOZI WA KIAFRIKA

         Katika kampeni zake za kuwania Uwaziri Mkuu, David Cameron, Msomi wa Siasa, Falsafa na Uchumi kutoka Chuo Kikuu Maarufu na Aghali Duniani cha Oxford alikuwa na sera thabiti za kuziendeleza taifa lake na wananchi wenzake ambapo katika kampeni zake alizikatia kaulimbiu ya "BIG SOCIETY" ambayo ni kama Flagship ambapo katika motto wake huo aliunakshi nakshi na mikakati madhubuti kama ifuatayo;

(a)Give societies more powers, localism&devolution.
(b)Encourage people to take active role in their communities, volunteerism.
(c)Transfer power from Central Govt to Local Govt.
(d)Support co-ops, mutual, charities, and social enterprises.
(e)Publish govt data (open/transparent govt) means to exists to generate develop and showcase new ideas to help people to come together in their neighbourhoodsto do good things.

       Ukitathmini kwa umakini, kwa mawazo kuntu na yasiyo na mgando harakati za bwana David dhidi ya nchi yake utagundua kuwa Wazungu na Waafrika wana tofauti katika uratibu, utendaji na utekelezaji wa mambo mbalimbali kama huamini fikiria kuwa ni kiongozi gani umewahi kumsikia katika kampeni zake akiwa na mawazo, fikra na mipango endelevu kwa wananchi wake? Hili la Cameron ni moja, mbili na tatu unayo wewe Mpenzi Msomaji...
     
       Nashindwa kumalizia makala hii bila kukuchopolea moja ya nukuu zake alizowahi kuongea katika kampeni zake ambazo zilikuja kumuweka kileleni hapa alipo sasa, alisema hivi...

                                "I got into politics because i love this country (Great Britain)"
                                                           David Cameron, Waziri Mkuu wa Uingereza.

No comments:

Post a Comment