Powered By Blogger

Thursday, March 8, 2012

NANI KAMA MESSI KATIKA KANDANDA?

Lionel Messi akiwa na shujaa wake Maradona
Bado akiwa kinda wa miaka 24, Lionel Messi aweka rekodi ya kufunga magoli matano wakati klabu ya Barcelona ilipoicharanga Bayer Leverkusen magoli 7-1 wakati wa mehi ya marudiano wa kutafuta tiketi ya kucheza duru ya 16 bora ya mashindano hayo. Barcelona wameifunga Bayer Leverkusen jumla ya magoli 10-2 kufuatia ushindi wa kwanza walioupata dhidi ya wapinzani hao magoli 3-1 katika mzunguko mashindano hayo makubwa duniani.

Safu hii hasa ni kwa mintaarafu ya shabaab Messi ambaye katika msimu wa mwaka 2008-9 aliifungia timu yake magoli 9 na  mengine 8 msimu uliofuata na kuifungia magoli ithnaashara wakati Barcelona ilipotwaa vikombe viwili ndani ya misimu mitatu ya mashindano hayo.

Lionel Messi ameweka rekodi kwa kushika nafasi ya pili ya wafungaji wa juu kabisa katika mashindano hayo ambapo aliye kileleni ni Mjerumani Gerd Muller aliyewahi kufanya hivyo wakati mashindano hayo yakiitwa European Cup.

Mjerumani Gerd Muller
Gerd Muller aliyekuwa mshambuliaji hatari wa klabu ya Bayern Munich iliowahi kushinda vikombe vitatu vya Champions League miaka ya 70 ambapo mwaka 72-73 alifunga magoli 11, 73-74 na 74-75 akifunga magoli 8 kwa kila msimu.

Mreno kutoka Msumbiji Eusebio
Mbali na gwiji huyo wa ujerumani, mshambuliaji wa Ureno, Eusebio naye aliweka rekodi ya kufunga magoli 9 kwa kila msimu katika misimu mitatu mfululizo. Wengine ni Jose Augustino Torres 64-65 aliyekuwa na magoli tisa akicheza klabu ya Benfica pamoja na shujaa Eusebio na mwaka uliofuata mchezaji mwingine Ferencvaros Florian Albert aliandika historia yake kwa kupachika magoli matano.

Source; Kwa msaada wa Mtandao

No comments:

Post a Comment