Powered By Blogger

Friday, February 17, 2012

MNAIJERIA UMAR MUTALLAB AFUNGWA JELA MAISHA

Kijana Umar akiwa ameweka pozi pembezoni mwa ukingo wa Mto Thames jijini London.
Akiwa bado kinda na kijana wa miaka 25, na shahada yake ya Uhandisi kutoka katika moja ya chuo kikuu kikongwe na maarufu cha UCL University College London alikohitimu jiwe lake hilo June, 2008, Kijana mtanashati, msomi kutoka katika familia ya kitajiri nchini Nigeria Umar Farouk Mutallab atatumia kudra alizojaliwa na Rabuka akiwa gerezani, kifungoni nchini Marekani.

Chupi iliyokuwa na bomu lililoshinda kuwasha kibiriti.
Umar alitaka kuishangaza dunia kwa kitendo chake cha kigaidi baada ya jaribio lake kushindwa kufua dafu Dec, 25, 2009 alipokuwa katika pipa lililokuwa linatoka jijini Amsterdam, Uholanzi na kukata mbingu ya Mungu kuelekea kwa Rais Obama katika jimbo la Michigan, Detroit ambapo lengo lilikuwa ni kuona safari yao ikigeuka majivu na watu kusaga meno huku maswahiba wakifurahi lakini Mungu si Athuman kwani kilipuko alichovaa katika kufuli kilishindwa kutimiza lengo lake baada ya wakaguzi wa ndege kumshukia kwa kuwa hakuwa katika hali ya utulivu.

Aliivaa chupi ambayo aliitegesha bomu ambalo lilishindwa kulipuka kwa manusura ya Mungu na kuokoa maisha ya abiria wapatao 253 katika ndege hiyo ya Northwest Flight Airlines

Kijana huyo wa Mutallab alijulikana kwa jina la Underwear Bomber kutokana na mkasa huo alihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na mashtaka nane ya kigaidi. Hukumu hiyo ambayo imwashtua wazazi wake na kuwapa wahka wakidai kuwa mahakama haina budi kufikiria upya uamuzi waliofanya kwa kijana wao kwa kosa hilo la kibinadamu.

Wakati akisoma hukumu hiyo siku ya alhamisi ya feb 16, 2012, Jaji wa Mahakama ya Wilaya ya Detroit Nancy Edmunds amesema kuwa Umar anastahili hukumu hiyo kutokana na kitendo hicho cha kigaidi.

Umar angekutwa na adhabu ya kifo laiti jaribio lake lingeng'arimu hata maisha ya abiria mmoja ilhali hukumu hiyo itaendana na ukosefu wa msamaha wa Rais yani Parole.

No comments:

Post a Comment