Kijana Umar akiwa ameweka pozi pembezoni mwa ukingo wa Mto Thames jijini London. |
Chupi iliyokuwa na bomu lililoshinda kuwasha kibiriti. |
Aliivaa chupi ambayo aliitegesha bomu ambalo lilishindwa kulipuka kwa manusura ya Mungu na kuokoa maisha ya abiria wapatao 253 katika ndege hiyo ya Northwest Flight Airlines
Kijana huyo wa Mutallab alijulikana kwa jina la Underwear Bomber kutokana na mkasa huo alihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na mashtaka nane ya kigaidi. Hukumu hiyo ambayo imwashtua wazazi wake na kuwapa wahka wakidai kuwa mahakama haina budi kufikiria upya uamuzi waliofanya kwa kijana wao kwa kosa hilo la kibinadamu.
Wakati akisoma hukumu hiyo siku ya alhamisi ya feb 16, 2012, Jaji wa Mahakama ya Wilaya ya Detroit Nancy Edmunds amesema kuwa Umar anastahili hukumu hiyo kutokana na kitendo hicho cha kigaidi.
Umar angekutwa na adhabu ya kifo laiti jaribio lake lingeng'arimu hata maisha ya abiria mmoja ilhali hukumu hiyo itaendana na ukosefu wa msamaha wa Rais yani Parole.
No comments:
Post a Comment