Powered By Blogger

Saturday, February 18, 2012

K-NEL AHABARISHA HASA KUHUSU ULAYA NA MAREKANI

 Mwanamuziki wa Rap na Mjasiriamali K-Nel akiwa mitamboni.
K-Nel ni mtangazaji wa kipindi cha Surprising Europe kinachorushwa hewani na runinga lililojizolea umaarufu duniani kwa kuanika uchafu wa mataifa yaliyoendelea Al-Jazeera ( Kisiwa) kilichokuwa na kitovu chake jijini Doha, Qatar mashariki ya kati.

Surprising Europe ni kipindi cheye chenye mlolongo wa habari za maisha ya waafrika waliohamia Ulaya na Marekani kihalali au kiharamu, na kuwaonyesha namna wamatumbi wanavyohangaika usiku na mchana wakisoma vyuo na kutafuta maisha kijumla huku wakipambana na hali ngumu ya uchumi wa kiliberali, utamaduni, hali ya hewa, ubaguzi wa rangi na upweke.

Kipindi kinachimba shimo kubwa hasa kwa kuwamulika waafrika na matatizo, mashakili na masaibu yao wakiwa katika nchi hizo za barafu na baridi kali zenye utofauti mkubwa na bara la afrika. Waafrika wanaonyeshwa namna wanavyofanya kazi chafu na za kidhalimu na kidhalili huku kipato chao kikishindwa kukidhi mahitaji ya kila siku, waafrika wanajiuza, wanasafisha vyoo, barabara, wanatembeza bidhaa, wanasuka nywele wazungu kwenye fukwe za bahari, wahudumu wa baa, wengine wakijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya na kuhatarisha maisha yao ili mradi mkono uende kinywani.

Pia kinahabarisha namna baadhi ya wamatumbi wanavyobaka na kufoji hati za kuishi ili wasisumbuliwe.
Surprising Europe ni kipindi elimu hasa kwa wote wenye ndoto za kwenda majuu kwa mintaarafu ya elimu, kutafuta maisha na bahati kadhalika za Dunia hii.

Alizaliwa jijini Nairobi, Kenya kama Nelson Mike Mithambo Miriuki kuanza mambo ya kunga ya uimbaji akiwa kinda wa miaka 4 akiimba nyimbo za kwaya, kuandika tamthiliya ndogo na mashairi.

Alipokuwa tineja akaingiwa na mdudu wa RnB na Hip Hop na kuwahusudu sana wanamuziki wa kimarekani marehemu Tupac Shakur, Big Poppa na shujaa wake wa muziki Jay Z.

K-Nel alihamia Ujerumani akiwa na miaka 19 kwa dhamira ya masomo ya Chuo Kikuu na mwaka 2004 na kuungana na Mama yake ambaye alikuwa akiishi huko muda mrefu. Alipakuwa jikoni albamu yake ya kwanza aliyoiita The Middle Finger na kubahatika kufanya kazi na msanii wa marekani Jay Z katika sherehe za sikukuu ya uhuru wa Kenya zilizofanyika Cologne mwaka huo.

Akiwa na kofia takribani tatu, utangazaji, muziki na ujasiriamali K-Nel anawaeleza waafrika wote wenye ndoto za kwenda majuu kuwa hawana budi kuarifiwa kabla hawajafunga mikanda yao kwani si kila ving'aavyo ni dhahabu.

Anauma na kupuliza kwani kauli mbiu yake kwa wamatumbi wanaohusudu Ulaya na Marekani ni kuwa

kwa maelezo zaidi... www.surprisingeurope.com

Friday, February 17, 2012

MNAIJERIA UMAR MUTALLAB AFUNGWA JELA MAISHA

Kijana Umar akiwa ameweka pozi pembezoni mwa ukingo wa Mto Thames jijini London.
Akiwa bado kinda na kijana wa miaka 25, na shahada yake ya Uhandisi kutoka katika moja ya chuo kikuu kikongwe na maarufu cha UCL University College London alikohitimu jiwe lake hilo June, 2008, Kijana mtanashati, msomi kutoka katika familia ya kitajiri nchini Nigeria Umar Farouk Mutallab atatumia kudra alizojaliwa na Rabuka akiwa gerezani, kifungoni nchini Marekani.

Chupi iliyokuwa na bomu lililoshinda kuwasha kibiriti.
Umar alitaka kuishangaza dunia kwa kitendo chake cha kigaidi baada ya jaribio lake kushindwa kufua dafu Dec, 25, 2009 alipokuwa katika pipa lililokuwa linatoka jijini Amsterdam, Uholanzi na kukata mbingu ya Mungu kuelekea kwa Rais Obama katika jimbo la Michigan, Detroit ambapo lengo lilikuwa ni kuona safari yao ikigeuka majivu na watu kusaga meno huku maswahiba wakifurahi lakini Mungu si Athuman kwani kilipuko alichovaa katika kufuli kilishindwa kutimiza lengo lake baada ya wakaguzi wa ndege kumshukia kwa kuwa hakuwa katika hali ya utulivu.

Aliivaa chupi ambayo aliitegesha bomu ambalo lilishindwa kulipuka kwa manusura ya Mungu na kuokoa maisha ya abiria wapatao 253 katika ndege hiyo ya Northwest Flight Airlines

Kijana huyo wa Mutallab alijulikana kwa jina la Underwear Bomber kutokana na mkasa huo alihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na mashtaka nane ya kigaidi. Hukumu hiyo ambayo imwashtua wazazi wake na kuwapa wahka wakidai kuwa mahakama haina budi kufikiria upya uamuzi waliofanya kwa kijana wao kwa kosa hilo la kibinadamu.

Wakati akisoma hukumu hiyo siku ya alhamisi ya feb 16, 2012, Jaji wa Mahakama ya Wilaya ya Detroit Nancy Edmunds amesema kuwa Umar anastahili hukumu hiyo kutokana na kitendo hicho cha kigaidi.

Umar angekutwa na adhabu ya kifo laiti jaribio lake lingeng'arimu hata maisha ya abiria mmoja ilhali hukumu hiyo itaendana na ukosefu wa msamaha wa Rais yani Parole.