Powered By Blogger

Thursday, September 8, 2011

"Hujafa Hujaumbika"- Wasemavyo Wahenga

Bwana Tony Nicklinson alivyo sasa
     Tony Nicklinson amepooza kuanzia kwenye shingo, baada ya kuugua kiharusi tangu mwaka 2005 alipokuwa safarini kibiashara nchini Austria.
Bwana Nicklinson amekuwa ni mtu wa kukaa ndani kutwa kuchwa hukumwili wake ukiwa hauwezi kusogea kwenda mahali popote isipokuwa akili yake ndo inayoendelea kufanya kazi kwa kuweza kuzungusha macho ya kutikisa kichwa basi.

     Tony ambaye alikuwa ni Mhandisi huishi na mkewe Bibi Jane Nicklinson ambaye ndiye anayemsaidia kwa kumuogesha, kumvalisha na kumlisha huku akimwendesha katika baiskeli ya walemavu  na pia kumwekea kisanduku cha herufi kiitwacho Perspex Box atakapo kuongea jambo na maneno yale huandikwa katika kifaa maalum wa njia ya ujumbe

   Ana umri wa miaka 57 sasa na amekuwa akiuguzwa nyumbani kwake kwa takribani miaka sita huku akilaumu kuwa amechoshwa na maisha yake kwani anahisi ni mateso na anapenda sheria za Uingereza zinabadilishwa ili aweze hata kuuawa ili apate kupumzika Right of Private Life au Suicide Legal
Sheria nchini Ungereza haziruhusu mtu kujiua, hivyo bwana Nicklinson amekuwa akishutumu sheria hiyo kuwa humnyima mtu uhuru wa kutotaka kuendelea kuishi.

    Akijibu swali hilo kwa mwandishi wa habari wa BBC Stephen Tackur kupitia kipini cha mahojiano cha Hardtalk  Bi Jane Nicklinson amesema kuwa endapo sheria hiyo haitapitishwa nchini humo basi hatokuwa na budi kwenda nchini Switzerland ambapo  mumewe ataweza kuruhusiwa  kufanyiwa Mercy Kiling ili kuepuka adha na fadhaa anazoendelea kuzipata mumewe huyo aliyebarikiwa kupata naye watoto wakike wawili ambao wanajitegemea
Mke wa bw. Nicklinson Jane Nicklinson
Bi Jane pia amekiri katika mahojiano hayo kuwa yu tayari kumuona mumewe akiuawa kwani maisha yake humpa huzuni na majonzi sana akikumbuka kipindi alipokuwa mzima wakisafiri pamoja ulimwenguni kote, hakika humuumiza sana mtima wake.

   Pomoja na kupooza ila Bwana Nicklinson  anaandika historia ya maisha  yake ( MEMOIRS) kabla hajapata kupooza na mapaka sasa alivyo.
Bwana Tony Nicklinson anaishi na mkewe mpendwa Bi Jane Nicklinson kwa miaka 24 sasa na wana mabinti wawili Lauren 22 na Beth  21 wote wakiishi huko Chippenham, Wiltshire.

    Tony Niclinson alikuwa meneja wa ukakiki wa ubora katika Kampuni la Uhandisi la Ugiriki lililokuwa likifanya shughuli zake  katika nchi za jumuiya za falme za kiarabu (UAE) wanadai alikuwa mchapakazi na mwenye nguvu.


    Maisha ya Bwana Tony Nicklinson hutukumbusha methali ya Wahenga inenayo kuwa “ Hujafa Hujaumbika Mwana-adam”

    Source: Hard Talk,  BBC World Service