Bwana Tony Nicklinson alivyo sasa |
Bwana Nicklinson amekuwa ni mtu wa kukaa ndani kutwa kuchwa hukumwili wake ukiwa hauwezi kusogea kwenda mahali popote isipokuwa akili yake ndo inayoendelea kufanya kazi kwa kuweza kuzungusha macho ya kutikisa kichwa basi.
Tony ambaye alikuwa ni Mhandisi huishi na mkewe Bibi Jane Nicklinson ambaye ndiye anayemsaidia kwa kumuogesha, kumvalisha na kumlisha huku akimwendesha katika baiskeli ya walemavu na pia kumwekea kisanduku cha herufi kiitwacho Perspex Box atakapo kuongea jambo na maneno yale huandikwa katika kifaa maalum wa njia ya ujumbe
Ana umri wa miaka 57 sasa na amekuwa akiuguzwa nyumbani kwake kwa takribani miaka sita huku akilaumu kuwa amechoshwa na maisha yake kwani anahisi ni mateso na anapenda sheria za Uingereza zinabadilishwa ili aweze hata kuuawa ili apate kupumzika Right of Private Life au Suicide Legal
Sheria nchini Ungereza haziruhusu mtu kujiua, hivyo bwana Nicklinson amekuwa akishutumu sheria hiyo kuwa humnyima mtu uhuru wa kutotaka kuendelea kuishi.
Akijibu swali hilo kwa mwandishi wa habari wa BBC Stephen Tackur kupitia kipini cha mahojiano cha Hardtalk Bi Jane Nicklinson amesema kuwa endapo sheria hiyo haitapitishwa nchini humo basi hatokuwa na budi kwenda nchini Switzerland ambapo mumewe ataweza kuruhusiwa kufanyiwa Mercy Kiling ili kuepuka adha na fadhaa anazoendelea kuzipata mumewe huyo aliyebarikiwa kupata naye watoto wakike wawili ambao wanajitegemea
Mke wa bw. Nicklinson Jane Nicklinson |
Pomoja na kupooza ila Bwana Nicklinson anaandika historia ya maisha yake ( MEMOIRS) kabla hajapata kupooza na mapaka sasa alivyo.
Bwana Tony Nicklinson anaishi na mkewe mpendwa Bi Jane Nicklinson kwa miaka 24 sasa na wana mabinti wawili Lauren 22 na Beth 21 wote wakiishi huko Chippenham, Wiltshire.
Tony Niclinson alikuwa meneja wa ukakiki wa ubora katika Kampuni la Uhandisi la Ugiriki lililokuwa likifanya shughuli zake katika nchi za jumuiya za falme za kiarabu (UAE) wanadai alikuwa mchapakazi na mwenye nguvu.
Maisha ya Bwana Tony Nicklinson hutukumbusha methali ya Wahenga inenayo kuwa “ Hujafa Hujaumbika Mwana-adam”
Source: Hard Talk, BBC World Service